Wednesday 16 November 2011

Kubadilisha taste ya perfume


Imekuwa ni kawaida ya perfumista wengi kupendelea kutumia perfume fulani kwa sababu wamekuwa wakiitumia kwa muda mrefu na wanaamini inawafanya wanukie na kujisikia vizuri. Kwa hiyo unakuta mtu anaendelea kununua perfume ile ile over and over again. Sio vibaya kuendelea kutumia kama unaipenda ila ni vizuri pia kuchanganya na nyingine wakati mwingine.

Well, kadri siku zinavyokwenda vitu around you vinabadilika hii ni permoja na umri, kazi au lifestyle kwa ujumla hata taste ya perfume inabadilika.Unaweza kupenda perfume fulani kwa sababu kila mtu mjini anaitumia, wakati mwingine sio vibaya kwenda kwenye mkusanyiko wa watu ukiwa unanukia attractive lakini kivyako.

At te end of the day, unapotumia perfume si kwa ajili ya  kuwafurahisha watu wengine, ila kutumia perfume inayokupendeza na kukufurahisha wewe. Kwa hiyo usijali kutumia perfume ambayo watu hawai-recognise ili mradi unaacha kumbukumbu nzuri.

Perfume iko kwa ajili ya kuelezea wewe ni mtu wa aina gani na ni therapy ambayo haihitaji therapist kwa hiyo lipuka na scent uipendayo kwa muda uupenda na mahali upendapo utajisikia vizuri muda wote.



                                                 Express yourself with scents

Unakaribishwa kutoa maoni yako kuhusiana na hili au linginelo, siku njema.

2 comments:

  1. duka lako liko wapi sasa? umepost tu hapa ila hujasema ulipo

    ReplyDelete
  2. perfume zinapatikana duka linaitwa dallas liko sinza kijiweni karibu

    ReplyDelete