Friday 11 November 2011

zawadi zetu za chrismas zinaendelea

Pata ideal gift yako iwe kuji-treat mwenyewe au kwa ajili ya wapendwa wako. Wahi kabla hazijaisha christmas imekaribia, dont leave to last minute.

Kwa kuwarahisishia wateja wetu perfume zote na gift set sasa zinapatika Dallas duka la vitu za ukweli lililopo sinza kijiweni karibu na duka la nguo la kwa wajanja. Wa kariakoo kaeni mkao wa kula zinakuja upande wenu.

Vile vile unaweza pata huduma kupitia simu namba 0716199724 au email imafmtz@gmail.com kama kawa

Utajisikiaje ukiamka asubuhi siku ya christmas ukakutana na kitu kama hiki maalum kwa ajili yako, that's all I wish for chrismas.
                                                            KARIBUNI

Thursday 10 November 2011

Tangazo la perfume ya Marc Jacobs Oh, Lola! labaniwa

Tangazo la perfume mpya ya Marc jacobs Oh, Lola! zimefungiwa na Advertising Standards Agency (ASA) kwa kuwa linasemekana kuwa sexually provocative. ASA wameangalia umri na mavazi ya model na position ya chupa katika kufanya maamuzi. Hii yuote ni katika kuwalinda watoto.



Je unafikiri tangazo limetendewa haki au wamewabania tu?

Ijumaa njema

Hot new high street scents

Nice and pricey Kama budget inaruhusu zisake pia
Guilty IntenseGucci guility Intense (Oriental) 50ml £59

ELIE SAAB LE PARFUMElie saab le parfum(Floral) 50m £60

TrĂ©sor Midnight RoseLancome Tresor midnight rose (floral) 50ml £49

Kama kawaida hizi ni high street brand kwa hiyo hizi price zinasababu zaidi ya quality ya perfume(waweza pitia older post FM ni nini kujua zaidi)

kwa nini usijaribu exceptional high quality Federico Mahora perfumes with same fragrance family kwa bei nafuu. You will never regret




Hii FM 320 na nyingine nyingiiii zote ziko tayari kuwa perfect gift kwa wapendwa wako christmas na mwaka mpya na zinakuja kwenye gift bag nzuriii. 

wasiliana nasi kwa maelezo zaidi, pia utapata msaada wa kuchagua signature perfume yako kutoka kwa perfumista mzoefu na mchangamfu kwa kujaribu sample zaidi ya 150 huwezi kosa unachotafuta iwe jinsia, age au occasion zote zipo.

email: imafmtz@gmail.com Piga simu namba 0716199724 (TZ)

KARIBUNI

Wednesday 9 November 2011

List ya top perfume kwa ajili ya zawadi ya chrismas na mwaka mpya

chagua perfume kwa style au fragrance family, easy! Ladies first

kwa mtu irresistible, perfect kwa kutumia jioni

FM317 (Floral) na

FM 32(Oriental)


Mwanamke yoyote aliye morden atapenda hii

FM 147 (Floral)

Inaendelea

Jinsi ya kuchagua perfume inayofaa kama zawadi 2 -TIPS

Kuna maelfu ya perfume madukani, lakini sio perfume zote ni nzuri kwa kila mtu, kwa hiyo ni muhimu kuchagua perfume ambayo itamfaa mtumiaji ili kuepuka disappointment.




kumbuka perfume nzuri ni ile inayomfanya mtumiaji kujisikia vizuri, kuongeza confidence na uchangamfu, na kusaidia kuexpress haiba na mood yake. Kwa hiyo chagua the best and right one. How?

Tips:

1. Usifanye haraka kununua perfume, chukua muda kutafuta perfume nzuri.

2. Ili uweze kupata perfect perfume jaribu kuchunguza ni perfume gani mlengwa anapendelea kwa kuangalia antumia perfume ipi  kwa sasa au anpenda kuongelea perfume gani. Unaweza pia chunguza personality au style yale (casual, classic, elegant nk) au occasion ( kwa ajili ya kazini, kutokea jioni, party au matumizi ya kila siku). hii iatakusaidia kuchagua kwani kuna perfume kusuit kila age, occasion, style au personality.

3. Usinunue perfume kwa kuchagua jina la perfume au brand name au muonekano tu no no no, kama hauijui kwani majina mengine ni matangazo tu na hai-reflect juice iliyopo ndani na inaweza isiendane na vigezo hapo no.2 ambavyo ni muhimu.

4. Tip muhimu kuliko zote ni kujaribu (smell perfume) Unataka kuchagua perfume ambayo utapenda mlengwa anukie vizuri. sio vibaya kununua perfume ambayo anayotari easy! ingawa ni vizuri zaidi kama utampatia perfume tofauti ambayo inaweza kuwa katika fragrance family moja na anayotumia sasa (floral, oriental, wood, citrus, chypre au fougere, kwa maelezo zaidi ya magroup haya na mengine pitia older post) kwa njia hii huwezi kuwa disappointed.

5. usisahau kufunga zawadi yako vizuri na kuongeza ujumbe wako, wao! hii itakuwa perfect gift isiyosahaulika, 100% sure.



List ya top perfume gift kwa ajili ya chrismas na mwaka mpya inakuja, utapitwaje?

Good luck

Jinsi ya kuchagua perfume inayofaa kama zawadi 1


Chrismas na mwaka mpya zimekaribia. kwa kawaida huu ni muda wa ndugu, jamaa na marafiki kupeana zawadi kama ishara ya upendo na kujali. Kama bado haujachagua ni zawadi gani ungependa kumpa umpendaye/unayemjali (awe mama, baba, mke, mme, mfanyakazi mwenzako, ndugu, jamaa au rafiki ) unaweza kuchagua perfume kama zawadi.



Kwa nini perfume?
Perfume ni chaguo zuri sana kwa zawadi (iwe chrismas, mwaka mpya, birthday, valentine's day, mother/father's day, kumwambia mtu unampenda/unamjali au kumpa pongezi)kwa sababu ni nzuri, zinatumika kila siku na haisahauliki.

kila mtu anapenda kunukia vizuri na kuvutia. Perfume inamfanya anayeitumia ajisikie vizuri, inaongeza confidence na kuelezea personality ya mtumiaji kama mwanamke au mwanaume. Fikiria kama unaweza kumfanya mtu ajisikie vizuri kwa kumpatia zawadi ya perfume tu. Kwa hakika atakukumbuka kila wakati atumiapo perfume uliyompa na kusiwa na kila anyekutana nae kuwa annukia vizuri. Wonderful!

Kitu kizuri kutumia perfume kama gift ni kwamba haiharibiki mwezi huu au ujao, inaweza tumiwa kila siku na kwa muda mrefu kabla haijaisha na sio rahisi mtu kuisahau uvunguni mwa meza kwani kila mtu anapenda kupamba perfume zake kwenye dressing table yake au sehemu inayoonekana. vilevile mtu hawezi kusema nina perfume za kutosha kwani ni vizuri kuwa na perfume zenye harufubtofauti ili upate ya kazini, kutokea, kushindia nyumbani nk au kunukia tofauti kila siku kuliongana na mood.


Pitia tips za kuchagua perfume ili uweze chagua perfume inayomfaa unayempa zawadi

Endelea kuwepo

Tuesday 8 November 2011

Macelebrity wa bongo nao kutoa perfume zao, hata Lady Gaga analeta yake!

Ni muda sasa tangu superstars mbalimbali kuanzia footballers (David Beckam), wanamitindo (Naomi Campbell), wacheza cinema na wanamuziki wengiii ambao nikiwataja siwezi kuwamaliza,wote kutoka majuu wamekuwa wakitumia majina na umaarufu wao kutoa perfumes ambazo zimekuwa ziki-hit soko la perfume na kulipa.

Lady Gaga

Haya hata Lady gaga nae anatoa yake mwakani sambamba na Madonna. Inasemekana perfume ya gaga itaitwa Monster na itanukia kama damu na semen. Nahisi chupa itakuwa kama skeleton fulani hivi.

Wapi macelebrity wa bongo, zamu yenu sasa kutoa fragrance zenu, inawezekana. Namimi natengeneza fragrance composition yangu ikiwa tayari nitafanya deal na celebrity mmoja wa bongo, imekaajee.

HEAT For Women By BEYONCE Eau De Parfum Spray

Hii ni ya beyonce, tunasubiri ya superstar wa bongo

Monday 7 November 2011

PERFUME ZA UKWELI, WAHI YAKO KABLA HAZIJAISHA UNUKIEE

Bonyeza play arrow  na enjoy muonekano

Luxury Federico Mahora 296 perfume for her



Luxury Federico Mahora 294 perfume for her



Luxury Federico Mahora 295 perfume for her



Umependa , karibu unuse zinanukiaje na kuchagua yako, piga simu namba 0716199724

Madonna ku-launch perfume yake ya kwanza-Truth or Dare!

Pop star Madonna ametangaza kutoa perfume yake ya kwanza itakayoitwa Truth or Dare mwakani mwezi wa nne.

madonna


Imekuwa kawaida kwa macelebrity kutoa perfume zao na kuteka soko la perfume madukani.
Macebrity kama Mariah Carey, Jennifer Lopez, Kim Kardashian, Beyonce na wengine wengi tayari wana fragrance line zao siku nyingi.




Madonna perfume truth or dare
 
Madonna ambaye yuko obsessed na perfume (Perfumista), amekuwa akitaka kutoa perfume ambayo ni personal kwake na inamuelezea yeye na bado ikawagusa watu wengine vilevile. How nice.
 
Perfume yake inawakilisha honest na daring ndio maana inaitwa TRUTH or DARE.
 
Apparently inanukia kama perfume aliyokuwa akitumia mama yake na huko ndiko alikopata inspiration, nani kama mama! Madonna anailezea perfume yake kama something classic, timeless, modern, feminine, mysterious and fresh.
 
I can't wait to smell it.

Sunday 6 November 2011

Eid Mubarak Perfumistas

best perfume ads

 Week end njema perfumista







Usisahau kutumia perfume uipendayo katika kukamilisha muonekano wako kulingana na wakati au occasion ofcourse ku-emphasise personality yako.
You will never go unnoticed, attraction, attraction and more attraction just like teh ads above!!